Twiga Stars yatupwa nje WAFCON 2024

Joel JJ By Joel JJ β€’ 15th July 2025


Twiga Stars yatupwa nje WAFCON 2024

Timu ya taifa ya wanawake ya Tanzania, maarufu kama Twiga Stars, imehitimisha safari yake katika michuano ya WAFCON 2024 baada ya kuondolewa rasmi kufuatia kipigo cha mabao 4-1 dhidi ya Ghana katika mchezo wa mwisho wa hatua ya makundi uliochezwa nchini Morocco.

Katika mchezo huo wa mwisho wa kundi C, Twiga Stars ilikuwa na kazi moja t, kupata ushindi ili kujiweka hai kwenye mashindano, lakini matumaini hayo yalizimwa na vijana wa Ghana waliotawala mchezo kwa kiasi kikubwa.

Bao pekee la Twiga lilifungwa na Stumai Abdallah, huku Ghana wakifunga kupitia kwa Pricella Adubea, Alice Kusi, Evelyn Badu, na Chantelle Boye.

Kwa matokeo hayo, Twiga Stars imemaliza hatua ya makundi ikiwa nafasi ya mwisho kwenye kundi C kwa pointi moja tu waliyoipata baada ya kutoka sare dhidi ya Banyana Banyana ya Afrika Kusini.

Afrika Kusini imemaliza kileleni mwa kundi hilo kwa pointi saba, ikifuatiwa na Ghana yenye pointi nne sawa na Mali, lakini Ghana wakinufaika kwa uwiano mzuri wa mabao na hivyo kusonga mbele.

Hii inaashiria safari ngumu kwa Twiga Stars, ambayo licha ya jitihada zao, haikuweza kufanikisha malengo ya kuvuka hatua ya makundi kwenye mashindano haya makubwa ya bara la Afrika.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.