Local,Normal News,Yanga

Yanga kutumia michuano ya CHAN kusajili

Joel JJ By Joel JJ
16 Jul 2025
Yanga kutumia michuano ya CHAN kusajili

Yanga inatarajiwa kutumia michuano ya CHAN 2024 itakayoanza August 02 hadi August 30 kusaka wachezaji mahiri wa kuwasajili, imefahamika

Akizungumza hivi karibuni, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga Ali Kamwe alisema usajili wa timu hiyo umekamilika kwa asilimia 85

Kigogo mmoja wa Yanga amenukuliwa na Mwanaspoti,  akibainisha kuwa wataacha nafasi chache ili kuangalia wachezaji wengine kwenye michuano ya CHAN akieleza shida kubwa ni kupata mastaa wenye ubora lakini suala la fedha si tatizo kwao.

Kwa mujibu wa bosi huyo, walichopanga ni kwa baadhi ya nafasi wanazotaka kuziboresha kwenye kikosi chao watakuwa na mkakati maalum wa kuangalia watu bora watakaopatikana kwenye fainali hizo.

Bosi huyo wa juu Yanga anayehusika kwenye usajili, alisema wachezaji wote wanaoshiriki fainali hizo, ni wale wanaocheza ligi za ndani Afrika, hivyo wanaona hakutakuwa na ugumu mkubwa kwao kuwapata.

“Hatuwezi kumaliza nafasi zote, tutakuwa na jicho letu kwenye hizi Fainali za CHAN, unajua shida yetu sisi ni watu bora tunaowataka, sio fedha"

“Kama ingekuwa fedha tusingeingia sehemu ambazo kuna timu unaambiwa inazunguka na mchezaji ikiongea naye, tunataka watu sahihi kwa malengo yetu"

“Kuna wachezaji tutawatafuta kwenye fainali hizi, tumejipanga kwenda Uganda, Kenya na hapa nchini kufuatilia kwa kina wachezaji bora tunaowataka,” alisema

Michuano hiyo inafanyika katika kipindi ambacho dirisha la usajili liko wazi kwani litafungwa Septemba 7 huku michuano hiyo ikitarajiwa kufika tamati August 30

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE →
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
2h ago
READ MORE →
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE →
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE →
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE →
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE →
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE →
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE →
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE →
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE →