Kiungo wa Yanga Khalid Aucho huenda asiwe sehemu ya kikosi cha mabingwa hao wa kihistoria msimu ujao baada ya majadiliano ya kuhuisha mkataba wake kutofikia mwafaka, imefahamika
Yanga ilikuwa tayari kumpa Aucho mkataba wa mwaka mmoja lakini kiungo huyo hayuko tayari kuongeza mwaka mmoja, akihitaji mkataba wa miaka miwili
Mtu wa karibu wa Aucho ambaye ni mwanahabari, amesema Aucho huenda akaelekea Vietnam alikopata ofa nono zaidi
"Baada ya kikao cha wiki nzima, mimi kama Mwanahabari niliyekuwa na nafasi ya kuyaongea kutoka kwake na uongozi wa Yanga, rasmi Aucho hatokuwa na Yanga"
"Aucho anaweza kwenda Vietnam, kuna klabu ya Ligi Kuu ya huko imemuhitaji, naweza kusema Aucho hatakuwepo nchini msimu ujao," alisema Justine Kessy
Awali Yanga ilikuwa na makubaliano na Aucho kumuongeza mkataba wa mwaka mmoja lakini huenda fundi huyo kutoka Jinja akawa amebadili mawazo baada ya kushawishiwa na ofa kutoka nje
Katika eneo analocheza Aucho, Yanga tayari imemsajili kiungo Mohamed Doumbia huku pia ikihusishwa kukamilisha usajili wa kiungo kutoka CS Sfaxien Moussa Balla Conte



