Kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ kimemaliza kambi yake nchini Misri waliyokaa kwa siku 10 na kimerejea Tanzania leo
Kikosi hicho kabla ya kucheza mchezo wa ufunguzi wa CHAN dhidi ya Burkinafaso kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, itacheza mechi tatu za kirafiki kwenye uwanja wa Black Rhino, Karatu
Stars itacheza dhidi ya Senegal, Kenya na Uganda katika mashindano madogo ya CECAFA yaliyoandaliwa na Shirikisho hilo kwaajili ya kuziweka sawa timu hizo kwenye mashindano ya CHAN
Tanzania itafungua michuano hiyo August 02 katika mchezo wa ufunguzi dhidi ya Burkina Faso ambao utapigwa uwanja wa Benjamin Mkapa
Kabla ya mchezo huo, kutafanyika shamrashamra za ufunguzi wa michuano hiyo katika uwanja wa Benjamin Mkapa



