Simba yashusha mbadala wa Zimbwe Jr

Joel JJ By Joel JJ β€’ 20th July 2025


Simba yashusha mbadala wa Zimbwe Jr

Simba iko katika hatua za mwisho kukamilisha usajili wa mlinzi wa kushoto Khadim Diaw anayetua kutoka klabu ya Al Hilal

Diaw anachukua nafasi ya Mohammed Hussein aliyeachwa baada ya mchakato wa kumuongezea mkataba kukwama

Diaw sasa anakwenda kuwa chaguo la kwanza katika safu ya ulinzi upande wa kushoto

Khadim Diaw ni miongoni mwa wachezaji muhimu katika kikosi cha Al Hilal akicheza kwa mafanikio makubwa.

Msimu uliopita, alikuwa sehemu ya kikosi kilichofika hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika, na mchango wake uliisaidia timu hiyo kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Mauritania, licha ya kuwa walialikwa kushiriki ligi hiyo.

Huu ni usajili muhimu kuelekea msimu ujao hasa kutokana na uzoefu wake mkubwa katika soka la kimataifa barani Afrika.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.