International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Jumatano Julai 23 2025

Joel JJ By Joel JJ
β€’
23 Jul 2025
Tetesi za usajili Ulaya, Jumatano Julai 23 2025

Winga wa Real Madrid na Brazil Rodrygo, 24, ni mmoja wa nyota wa kumrithi Luis Diaz huko Liverpool iwapo winga huyo wa Colombia mwenye umri wa miaka 28 ataondoka Anfield (Florian Plettenberg).

Mshambuliaji wa Sweden Alexander Isak, 25, anataka pauni 300,000 kwa wiki kusaini mkataba mpya Newcastle (Talksport).

Granit Xhaka amekubaliana masharti na Sunderland, huku klabu hiyo sasa ikiwa kwenye mazungumzo na Bayer Leverkusen kuhusu ada ya kiungo huyo wa Uswisi mwenye umri wa miaka 32 (Times).

Atalanta na Lazio wanavutiwa na mshambuliaji wa Manchester United na Denmark Rasmus Hojlund, 22 (Footmercato).

Atletico Madrid wameanza mazungumzo na Chelsea kuhusu mpango wa kumsajili Renato Veiga, huku Blues wakidai takriban pauni milioni 35 kumuachia beki huyo wa kati wa Ureno mwenye umri wa miaka 21 (Fabrizio Romano).

Everton wanavutiwa na beki wa kushoto wa Bayern Munich na Morocco Adam Aznou, 19 (Athletic).

Brentford wamekataa ofa ya kwanza ya pauni milioni 30 kutoka Newcastle kwa ajili ya mshambuliaji wa DR Congo Yoane Wissa, 28 (Tbrfootball).

Wolves wako karibu kukamilisha usajili wa winga wa Colombia Jhon Arias, 25, kutoka Fluminense na beki wa kulia wa Hispania Marc Pubill, 22, kutoka Almeria (Telegraph).

Manchester United wanamfuatilia beki wa kushoto wa Mali, Dan Sinate wa Angers, lakini hawana uwezekano wa kufanya uhamisho kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 19 hadi Januari mapema zaidi (Sun).

Everton wanavutiwa na Samuel Lino wa Atletico Madrid, huku klabu hiyo ya Hispania ikiwa tayari kupokea ofa kwa winga huyo wa Brazil mwenye umri wa miaka 25 (AS).

BBC

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’