Simba yafunguka mipango ya pre-season

Joel JJ By Joel JJ β€’ 24th July 2025


Simba yafunguka mipango ya pre-season

Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Simba Ahmed Ali amesema mipango ya maandalizi ya msimu mpya 'pre-season' inaendelea ambapo klabu itaanza maandalizi ya awali hapa nchini kabla ya kusafiri nje ya nchi

Ahmed amesema mwishoni mwa mwezi huu wachezaji watarejea kambini kwa ajili ya taratibu za awali za maandalizi hayo

"Kwa wachezaji ambao tunaendelea nao nafikiri wao tayari wameanza kurejea, kwa hawa wpya tunatarajia hadi kufikia mwishoni mwa mwezi huu wataripoti kwa ajili ya hatua za awali za maandalizi yetu ya pre-season"

"Nafikiri tutaanzia hapa nchini kabla ya kusafiri nje ya nchi, baadae tutatoa taarifa juu wapi timu itakwenda kuweka kambi," alisema Ahmed

Awali Simba ilipanga kuanza pre-season Ijumaa ya Julai 25, lakini ni kama zoezi hilo limesogezwa mbele kwa siku chache

Habari njema ni kuwa bado kuna muda wa kutosha wa kufanya maandalizi kwani ligi zinatarajiwa kurejea katikati ya mwezi Septemba 2025

Michuano ya CHAN 2024 imepelekea mabadiliko hayo ikifanyika kuanzia August 02 hadi August 30


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.