Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Simba Ahmed Ali amesema mipango ya maandalizi ya msimu mpya 'pre-season' inaendelea ambapo klabu itaanza maandalizi ya awali hapa nchini kabla ya kusafiri nje ya nchi
Ahmed amesema mwishoni mwa mwezi huu wachezaji watarejea kambini kwa ajili ya taratibu za awali za maandalizi hayo
"Kwa wachezaji ambao tunaendelea nao nafikiri wao tayari wameanza kurejea, kwa hawa wpya tunatarajia hadi kufikia mwishoni mwa mwezi huu wataripoti kwa ajili ya hatua za awali za maandalizi yetu ya pre-season"
"Nafikiri tutaanzia hapa nchini kabla ya kusafiri nje ya nchi, baadae tutatoa taarifa juu wapi timu itakwenda kuweka kambi," alisema Ahmed
Awali Simba ilipanga kuanza pre-season Ijumaa ya Julai 25, lakini ni kama zoezi hilo limesogezwa mbele kwa siku chache
Habari njema ni kuwa bado kuna muda wa kutosha wa kufanya maandalizi kwani ligi zinatarajiwa kurejea katikati ya mwezi Septemba 2025
Michuano ya CHAN 2024 imepelekea mabadiliko hayo ikifanyika kuanzia August 02 hadi August 30



