Klabu ya Yanga imethibitisha kuachana na wachezaji watano ambapo miongoni mwao wamemaliza mikataba
Katika orodha hiyo yumo kiungo Khalid Aucho aliyewatumikia Wananchi kwa misimu minne
Aucho anaondoka Yanga huku bado ni kipenzi cha mashabiki kutokana na kazi nzuri aliyofanya katika misimu minne
Ameshinda mataji manne ya ligi kuu, mataji manne ya kombe la FA, mataji matatu ya Ngao ya Jamii na pia akiisaidia Yanga kufanya vyema katika michuano ya Kimataifa
Katika orodha hiyo pia yumo kiungo Clatous Chama aliyeitumikia Yanga kwa msimu mmoja akitokea klabu ya Simba
Kiungo Jonas Mkude nae amepewa Thank You baada ya mkataba wake kumalizika kama ilivyo kwa Kennedy Musonda aliyetimkia Israel
Stephane Aziz Ki yeye amejiunga na klabu ya Wydad Athletic, Yanga ikifanya biashara



