Aucho, Chama rasmi waachwa Yanga

Joel JJ By Joel JJ β€’ 24th July 2025


Aucho, Chama rasmi waachwa Yanga

Klabu ya Yanga imethibitisha kuachana na wachezaji watano ambapo miongoni mwao wamemaliza mikataba

Katika orodha hiyo yumo kiungo Khalid Aucho aliyewatumikia Wananchi kwa misimu minne

Aucho anaondoka Yanga huku bado ni kipenzi cha mashabiki kutokana na kazi nzuri aliyofanya katika misimu minne

Ameshinda mataji manne ya ligi kuu, mataji manne ya kombe la FA, mataji matatu ya Ngao ya Jamii na pia akiisaidia Yanga kufanya vyema katika michuano ya Kimataifa

Katika orodha hiyo pia yumo kiungo Clatous Chama aliyeitumikia Yanga kwa msimu mmoja akitokea klabu ya Simba

Kiungo Jonas Mkude nae amepewa Thank You baada ya mkataba wake kumalizika kama ilivyo kwa Kennedy Musonda aliyetimkia Israel

Stephane Aziz Ki yeye amejiunga na klabu ya Wydad Athletic, Yanga ikifanya biashara


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.