Klabu ya KMC inatarajiwa kumtangaza kocha Marcio Maximo kuwa mkufunzi wa timu hiyo
Maximo aliyewahi kuifundisha timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' na klabu ya Yanga, tayari yuko jijini Dar es salaam
Shamra shamra za kocha huyo raia wa Brazil huenda zikajiri leo pale Manispaa ya Kinondoni
Baada ya kupata mafanikio wakati akiinoa timu ya Taifa, hatimaye Maximo amerejea tena kwa mara ya tatu baada ya awamu yake ya pili na Yanga kutompa mafanikio makubwa



