Kikosi cha Simba kinatarajiwa kuondoka nchini kesho Jumatano kuelekea Misri kuanza maandalizi ya msimu mpya wa mashindano, 2025/26
Taarifa iliyotolewa na Simba mapema leo, imebainisha kuwa timu itaondoka Alfajiri, kambi hiyo ikitarajiwa kuwa mji wa Ismailia
Wachezaji wapya wanaungana na wenzao wanaoitumikia Simba tangu msimu uliopita kuelekea katika kambi hiyo
Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba Ahmed Ali amesema nyota pekee watakaokosekana katika kambi hiyo ni wale walio katika majukumu ya timu za Taifa kushiriki michuano ya CHAN inayoanza mwishoni mwa wiki
Simba inatarajiwa kuhitimisha kambi yake August 28 na kurejea nchini tayari kwa msimu mpya wa mashindano mbalimbali



