Local,Transfer News,Azam, Yanga, Simba

Azam Fc yaeleza ugumu wa kumuuza Fei Toto Simba

Joel JJ By Joel JJ
β€’
29 Jul 2025
Azam Fc yaeleza ugumu wa kumuuza Fei Toto Simba

Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa klabu ya Azam FC, Thabit Zacharia maarufu kama Zakazakazi, amefunguka kuhusu sababu zinazowazuia kumuuza kiungo mshambuliaji Feisal Salum Fei Toto kwa klabu ya Simba SC.

Kupitia mahojiano aliyofanya na redio moja maarufu jijini Dar es salaam, Zakazakazi alisema wazi kuwa Azam FC haiwezi kumuuza mchezaji huyo kwa Simba kutokana na kipengele maalum kilichopo kwenye mkataba wao na klabu ya Yanga, walipomnunua mchezaji huyo awali.

"Hatuwezi kumuuza Feisal kwenda Simba kwa sababu sidhani kama Simba wana pesa za kuweza kumnunua Feisal," amesema.

Zakazakazi ameweka wazi kuwa wakati Azam FC ilipomsajili Feisal kutoka Yanga SC, walikubaliana kuwa endapo mchezaji huyo atauzwa kwa Simba, basi Azam italazimika kuilipa Yanga fidia ya shilingi bilioni moja za Kitanzania.

"Wakati tunamchukua Feisal kutoka Yanga, yapo makubaliano ya kimkataba kuwa endapo tutamuuza mchezaji huyo kwa klabu ya Simba, tunapaswa kuilipa Yanga Tsh Bilioni 1," alifichua.

Ameongeza kuwa ili kufanikisha uhamisho huo, Simba italazimika kutoa dau kubwa litakalowezesha Azam kupata faida zaidi ya fidia hiyo, jambo ambalo linaonekana kuwa gumu.

"Sasa Simba watalipa shilingi ngapi tufanye biashara? Sisi hatuko tayari kulipa Bilioni 1 kwa Yanga kama dau lao litakuwa dogo, na pia lazima walipe dau ambalo litatufanya tupate zaidi ya Yanga," alisisitiza.

Pamoja na mijadala mingi inayoendelea mitandaoni kuhusu tetesi za uhamisho wa Fei Toto kwenda Simba, Zakazakazi amesema hadi sasa hawajapokea ofa yoyote rasmi kutoka kwa Simba.

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
2h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’