Local,Normal News,Yanga, Simba, Azam, Fountain Gate, Singida BS

Morocco afunguka maandalizi ya Stars CHAN

Joel JJ By Joel JJ
β€’
30 Jul 2025
Morocco afunguka maandalizi ya Stars CHAN

Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Hemed Suleiman 'Morocco', amesema kikosi chake kimekamilika kwa asilimia 80, na kwamba zilizobaki atazimalizia siku chache kabla ya kuanza fainali za Mataifa ya Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN), Jumamosi wiki hii.

Akizungumza juzi baada ya kumalizika kwa mchezo dhidi ya Timu ya Taifa ya Senegal, ukiwa ni maalum kujiweka sawa kabla ya fainali za CHAN, zinazofanyika hapa nchini kwa ushirikiano na nchi za Kenya na Uganda, Morocco, alisema pamoja na ushindi walioupata, lakini bado timu yake ina mapungufu machache, ambapo atatumia siku chache zilizobaki kuyarekebisha.

Katika mchezo huo uliopigwa Uwanja wa Black Rhino, Karatu mkoani Arusha, Stars ilishinda mabao 2-1 dhidi ya Senegal, yakiwekwa wavuni na Abdul Suleiman Sopu na Ibrahim Hamad 'Bacca'.

"Tumemaliza mechi salama na tumefanikiwa kwa asilimia 80 kwa kile ambacho tulikipanga katika mechi hizi mbili tulizocheza huku."

"Bado kuna mambo hayajakaa vizuri, kuna maeneo ambayo tunahitaji kuyafanyia kazi, kabla hatujaanza mechi yetu ya ufunguzi wa CHAN Agosti 2," alisema Morocco.

Aliwahakikishia Watanzania kuwa hadi kufikia Jumamosi kila kitu kitakuwa tayari na wanatarajia kufanya vizuri katika mchezo wa ufunguzi dhidi ya Burkina Faso, utakaopigwa Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

"Tunaendelea kujipanga, tunarudi nyumbani, tuna siku nne za kurekebisha mapungufu yaliyojitokeza kwenye michezo hii miwili, japo tumeshinda, nadhani mpaka siku hiyo tutakuwa vizuri," alisema.

Ulikuwa ni mchezo wa pili kwa Stars kushinda, ambapo Jumanne iliyopita, ikiwa kwenye uwanja huo, ilitoa kipigo cha bao 1-0 dhidi ya Uganda Cranes, lililowekwa ndani ya wavu na Idd Selemani 'Nado', katika michuano maalum ya kujiandaa na fainali, iliyopewa jina la CECAFA 3 Nations Pre-CHAN.

Kikosi cha Stars kimerejea Dar es Salaam, kufanya maandalizi ya mwisho kabla ya mchezo wa ufunguzi, Jumamosi ijayo.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
5h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
9h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
11h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
13h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
15h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
15h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
16h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
18h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
21h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’