Simba imetambulisha usajili wa kiungo raia wa Senegal Alassane Kante (24) kutoka klabu ya CA Bizertin ya Tunisia
Kante ametua Msimbazi katika nafasi ya Fabrice Ngoma ambaye alipewa 'Thank You' baada ya mkataba wake kumalizika
Kante ni kiungo wa kati ambaye pia anaweza kutumika kama kiungo mkabaji au mchezeshaji
Simba iliweka kipaumbele usajili wa kiungo huyo ambapo kocha Fadlu Davids alimuhitaji ili kuimarisha safu ya kiungo cha ukabaji



