Jumamosi August 02 2025 timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' itaweka karata yake ya kwanza katika michuano ya CHAN 2024 itakapoikaribisha Burkina Faso katika mchezo wa ufunguzi wa michuano hiyo inayofanyika kwa mara ya kwanza katika ukanda wa Afrika Mashiriki katika nchi za Tanzania Bara, Zanzibar, Kenya na Uganda
Tanzania imepewa heshima ya kipekee kwani uzinduzi wa michuano hiyo utafanyika hapa nchini
Ni wazi CAF wameichagua Tanzania kuzindua michuano hiyo kutokana na hamasa ya mashabiki, Tanzania imejipambanua kwa mashabiki kujitokeza kwa wingi viwanjani
Tiketi zinaendelea kuuzwa hivyo kama hujakata tiketi yako, bado una siku mbili. Hili ni jambo letu kama Watanzania, hivyo tujitokeze kwa wingi kuiunga mkono timu yetu ya Taifa
Tanzania ni moja ya timu zinazopewa nafasi ya kufanya vizuri katika michuano hii kutokana na ubora wa kikosi chake
INAWEZEKANA kombe hili likabaki hapa Tanzania, kwa umoja, ushirikiano na sapoti ya Watanzania wote, INAWEZEKANA





