Jana usiku Yanga ilitambulisha usajili wa mshambuliaji Andy Boyeli raia wa DR Congo aliyekuwa akiitumikia klabu ya Sekhukhune ya Afrika Kusini
Kocha Mpya wa Yanga Romain Folz ndiye aliyependekeza usajili wa mshambuliaji huyo ambaye msimu uliopita aliifunga Sekhukhune mabao saba ligi kuu ya Afrika Kusini
Msimu wa 2022/23 Boyeli aliitumikia Power Dynamos ya Zambia ambapo alitwaa kiatu cha mfungaji bora baada ya kufunga mabao 18 huku akitwaa tuzo ya MVP
Boyeli ndiye mrithi wa Kennedy Musonda aliyetimkia Israel baada ya mkataba wake kumalizika



