Klabu ya Simba jana ilithibitisha kumsajili kiungo mshambuliaji Morice Abraham akitua kama mchezaji huru
Morice aliyerejea nchini mapema mwaka huu akitokea Serbia baada ya kuachana na FK Spartak ya nchini humo, alijumuishwa katika kikosi cha Simba kama sehemu yake ya majaribio

Aidha Wekundu hao wa Simba pia wamemnasa kiungo Hussein Semfuko kutoka klabu ya Coastal Union
Semfuko anatua Simba baada ya kung'ara katika kikosi cha Coastal Union msimu uliomalizika
Nyota hao wamejumuishwa katika kikosi cha Simba kilichoweka kambi y pre-season huko Misri



