Local,Normal News,Yanga, Simba, Azam, Fountain Gate, Singida BS

Stars jino kwa jino na Burkina Faso ufunguzi CHAN 2024

Joel JJ By Joel JJ
2 Aug 2025
Stars jino kwa jino na Burkina Faso ufunguzi CHAN 2024

Mashindano ya Mataifa ya Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN) yanatarajiwa kuanza rasmi leo , Agosti 02, 2025, kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam, ambapo Tanzania (Taifa Stars) itamenyana na Burkina Faso katika mchezo wa ufunguzi utakaoanza saa 2:00 usiku.

Tanzania inakuwa mwenyeji wa mashindano haya kwa mara ya kwanza katika historia, kwa kushirikiana na Kenya na Uganda kama waandaaji wenza wa michuano hiyo ya Afrika.

Mchezo wa leo unatarajiwa kuwa na ushindani mkali, huku makocha wa timu zote mbili wakiweka wazi dhamira zao kuelekea mchezo huo

Mkufunzi wa Stars Hemed Morocco amewataka Watanzania kujitokeza kwa wingi kuwaunga mkono akiwahakikishia kikosi chake kiko tayari kwa michuano hiyo

"Tupo Tayari, Tuna Kikosi imara. Tupo tayari kukutana na timu yoyote katika mashindano haya kutokana na aina ya kikosi nilichonacho. Tumefanya maandalizi ya kutosha na wachezaji wote wako fiti,” alisema Morocco katika mkutano na wanahabari

Kocha huyo ameongeza kuwa michezo ya kirafiki waliyocheza kabla ya mashindano imesaidia kupunguza presha kwa wachezaji, hasa chipukizi waliopo kwenye kikosi hicho.

“Wachezaji chipukizi wameonyesha kiwango kizuri na kushirikiana vyema na wazoefu. Tunaamini tunaweza kufanya vizuri na kuacha kombe nyumbani,” alisisitiza.

Akizungumza kwa niaba ya wachezaji wenzake, mlinda lango Aishi Manula alisema wanakwenda kupambana kulinda heshima ya nchi nyumbani

"Tutapambana Kulinda Heshima ya Nyumbani.Tunajivunia kucheza kwenye ardhi ya nyumbani. Tutapambana kuhakikisha tunashinda michezo yetu ya mwanzo,” alisema Manula. 

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
9h ago
READ MORE →
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
12h ago
READ MORE →
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
14h ago
READ MORE →
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
16h ago
READ MORE →
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
18h ago
READ MORE →
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
19h ago
READ MORE →
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
19h ago
READ MORE →
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
21h ago
READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
1d ago
READ MORE →
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE →