Local,Normal News,

Yanga yaweka malengo mapya 2025/26

Joel JJ By Joel JJ
β€’
4 Aug 2025
Yanga yaweka malengo mapya 2025/26

Rais wa Yanga Injinia Hersi Said amewataka wachezaji wa timu hiyo kusahau mafanikio waliyopata msimu uliopita na kuwekeza nguvu ili kufanya vyema zaidi msimu ujao 2025/26

Akizungumza katika semina iliyofanyika jijini Dar es salaam jana ambayo iliwakutanisha wachezaji, benchi la ufundi na viongozi, Hersi alisema mafanikio yote ya msimu uliopita yameingia kwenye historia na sasa kila kitu kinaanza upya

"Hii ni familia imara sana, familia hii imekuwa na mafaniko makubwa katika misimu minne iliyopita, tunashukuru kwa mafanikio hayo tuliyopata lakini niwahakikishie yote yamekuwa historia"

"Tunaachana na historia sasa tuna kazi ya kufanya. ni msimu mpya na wote tunaanza tukiwa kwenye mstari mmoja"

"Iwe timu iliyonusurika kushuka daraja msimu uliopita au mabingwa, wote tunaanza katika mstari mmoja"

"Tusahau yote tuliyofanya msimu uliopita, mabao tuliyofunga, asisti au idadi ya mechi tulizoshinda yote yamekuwa historia. sasa tunakwenda kukabiliana na msimu mpya," alisema Hersi

Kikosi cha Yanga kimeanza rasmi maandalizi yake kujiandaa na mikiki mikiki ya 2025/26 ambapo kocha Romain Folz atakuwa na takribani siku 10 za kujiandaa kabla ya mechi yake ya kwanza y pre-season dhidi ya Rayon Sports itakayopigwa August 15 huko Rwanda

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
8h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
11h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
13h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
15h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
17h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
18h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
18h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
20h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
23h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’