Baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Burkina Faso ambao umeiweka Tanzania kileleni mwa kundi B, wenyeji hao wa michuano ya CHAN leo tena wanashuka dimba la Benjamin Mkapa kumenyana na Mauritania katika mchezo utakaopigwa saa 2 usiku
Tanzania leo inazihitaji alama zote tatu ili kuendelea kujiweka katika nafasi nzuri ya kutinga hatua ya mtoano
Ili kuhakikisha Watanzania wanaujaza uwanja wa Benjamin Mkapa leo, watu 10,000 wa kwanza kuingia katika majukwaa ya Mzunguuko hawatalipa kiingilio, muhimu wawe na N-Card
Zitachezwa mechi mbili, ukilipia kiingilio cha mchezo kati ya Stars dhidi ya Mauritania, utatizama bure mchezo wa saa 11 kati ya Burkina Faso dhidi ya Afrika ya Kati




