Bao la dakika za jioni lililofungwa na Shomari Kapombe limeihakikishia timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mauritania
Ni mchezo wa raundi ya pili hatua ya makundi Stars ikiandikisha ushindi wa pili mfululizo na kujichimbia kileleni mwa kundi B baada ya kufikisha alama 6
Hata hivyo leo haikuwa rahisi, Mauritania iliweka ngome imara katika kujilinda na yalihitajika maarifa ya Kapombe kukimbia nyuma ya mabeki kuwahi krosi ya Iddi Nado kuandikisha bao hilo la ushindi
Ushindi huo unaifanya Tanzania kuandikisha rekodi mpya kwa kushinda mechi mbili na kufikisha alama 6 katika michuano ya CHAN
Baada ya ushindi huo, Tanzania imejiweka katika nafasi nzuri ya kutnga hatua ya mtoano
