International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Jumamosi August 09 2025

Joel JJ By Joel JJ
β€’
9 Aug 2025
Tetesi za usajili Ulaya, Jumamosi August 09 2025

Paris St-Germain wanatarajia ofa kutoka kwa Chelsea, Manchester United au Inter Milan kwa ajili ya mlinda lango wa Italia Gianluigi Donnarumma, 26. (ESPN)

Newcastle wanajipanga kuwasilisha ofa ya pauni milioni 30 kumnunua mshambuliaji wa Brentford mwenye umri wa miaka 28 kutoka DR Congo Yoane Wissa. (Times)

Newcastle wameanza mazungumzo na PSG kuhusu mpango wa kumnunua mshambuliaji wa Ufaransa Randal Kolo Muani, 26. (Florian Plettenberg)

The Magpies pia wanafikiria kumnunua mshambuliaji wa Porto na Uhispania Samu Aghehowa, 21, ili kuimarisha safu yao ya ushambuliaji. (Athletic)

Mshambuliaji wa Senegal Nicolas Jackson, 24, angependelea kusalia katika Ligi ya Premia ikiwa ataondoka Chelsea msimu huu wa joto na uwezekano wa kwenda Newcastle. (Sun)

Jackson angependa kuondoka Chelsea mwezi huu, huku AC Milan na Juventus pia zikiwa na nia ya kumsajili. (Mail)

Manchester United inataka kumsajili kiungo mkabaji na mlinda lango mpya sasa wamekamilisha kumsaka mshambuliaji wa Slovenia Benjamin Sesko, 22, kutoka RB Leipzig. (Telegraph)

Southampton wanahitaji angalau pauni milioni 50 kwa winga wao wa chini ya miaka 21 wa England Tyler Dibling, 19, huku Everton wakitarajia kufanya mchakato wa kumpata. (Liverpool Echo)

Klabu ya Ufaransa ya Lille inalenga kumnunua kwa mkopo mlinda langi wa Spurs raia wa Czech Antonin Kinsky. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 yuko kwenye rada iwapo mlinda mlango chaguo la kwanza, Mfaransa Lucas Chevalier, 23, atajiunga na PSG. (L'Equipe )

Brentford wana nia ya kumsajili winga wa Bournemouth Dango Ouattara. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Burkina Faso mwenye umri wa miaka 23 alicheza mechi 32 za Premier League akiwa na Cherries msimu uliopita. (Sky Sports)

Leeds United iliyopanda daraja hivi karibuni inavutiwa na kiungo wa kati wa Brighton mwenye umri wa miaka 20 Facundo Buonanotte. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Argentina pia anasakwa na Borussia Dortmund.(Yorkshire Evening Post)

BBC

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
7h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
11h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
12h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
14h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
17h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
17h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
17h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
19h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
23h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’