Local,Normal News,Yanga

Yanga, Wakala wavutana ofa za Mzize

Joel JJ By Joel JJ
β€’
11 Aug 2025
Yanga, Wakala wavutana ofa za Mzize

Sakata la usajili wa mshambuliaji wa Yanga SC, Clement Mzize, limechukua sura mpya baada ya viongozi wa klabu hiyo kuweka wazi msimamo wao: hawatauza mchezaji kwa mapendekezo ya wakala wake, bali kwa kuzingatia thamani halisi ya mchezaji katika soko na muda uliopo.

Jana, klabu ya Esperance kutoka Tunisia iliwasilisha ofa rasmi Jangwani kwa ajili ya kumsajili Mzize, lakini mabingwa hao wa Ligi Kuu Tanzania Bara waliikataa mara moja.

Ikumbukwe kuwa Yanga tayari walikuwa wamekubaliana na klabu ya Umm Salal ya Qatar kumuuza Mzize kwa kiasi cha dola 900,000. Hata hivyo, dili hilo limesimama kutokana na kutokuwepo kwa makubaliano binafsi kati ya mchezaji na klabu husika, chanzo kikuu kikiwa ni msimamo wa wakala wa Mzize ambaye hataki mteja wake ajiunge na timu hiyo ya Qatar.

Badala yake, wakala huyo alipendekeza Yanga wamruhusu Mzize kujiunga na Al Masry ya Misri, ingawa klabu hiyo iliwasilisha ofa ndogo ya dola 600,000, chini kwa kiasi kikubwa ya thamani iliyowekwa na Yanga.

Vyanzo vinaeleza kuwa wakala huyo hana uhusiano mzuri na uongozi wa Yanga, hali iliyochochea mivutano ya mara kwa mara. Hata pale Zamalek SC walipoonyesha nia ya kumsajili Mzize, mpango huo ulisitishwa baada ya gharama upande wa mchezaji kuongezeka kinyume na makubaliano ya awali.

Kwa sasa, hatma ya Mzize inasalia kuwa yenye sintofahamu, huku Yanga wakisisitiza kuwa maslahi ya klabu na heshima ya mchezaji ndiyo kipaumbele na si masharti ya wakala.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
7h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
11h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
12h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
14h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
16h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
17h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
17h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
19h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
23h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’