Local,Normal News,Yanga

Yanga yasaini mkataba wa mabilioni SportPesa

Joel JJ By Joel JJ
11 Aug 2025
Yanga yasaini mkataba wa mabilioni SportPesa

Kampuni ya ubashiri wa michezo, SPORTPESA leo imesaini mkataba wa miaka mitatu kuendelea kudhamini klabu ya Yanga

Mkataba huo wenye thamani ya Tsh Bilioni 21.7, umesainiwa Serena Hotel jioni ya leo Jumatatu

Akizungumza katika hafla hiyo, Mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi SportPesa Mh. Tarimba Abbas alibainisha kuwa klabu ya Yanga itavuna takribani Billion 7.2 kila mwaka na kama ikibeba ubingwa wa Afrika watatoa bonasi ambayo hakuna klabu imewahi kuipata nchini

“Dhamira ya Sportpesa ilikuwa na ndoto kuingia kwenye mpira. Tuliwahi kudhamini Arsenal, Hully City, Everton, Ligi Kuu Kenya klabu kadhaa. Tulipotazama Tanzania tukabaini Yanga ni Klabu sahihi kutimiza nayo ndoto zetu. Yanga ina mashabiki wengi. Tuliwaamini sana viongozi wa Yanga kwamba tungeubadilisha mpira wa Tanzania”

"Baada ya sisi kuingia Yanga, tuliwapa nguvu ya kiuchumi. Yanga imekuwa na misuli ya kumsajili mchezaji kutoka klabu yoyote. Hii imefanya Yanga iwe na uwezo wa kumuuza mchezaji yoyote kwa sababu ina uwezo wa kumsajili mchezaji yeyote".

"Leo tumesaini mkataba mpya wa miaka mitatu. Mkataba huu ni Tshs bilion 21.7 Mkataba huu utaifanya Yanga iwe na ndoto ya kuwa Bingwa wa AFRIKA. Nje ya udhamini huu, Sportpesa Tumeweka Bonasi Kubwa kwenye mechi za kimataifa,” alisema Tarimba

Mgeni rasmi Nabu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma aliipongeza SportPesa na klabu ya Yanga kwa kuendeleza ushirikiano wao uliodumu kwa miaka nane ukiwa na tija kwa pande zote

“Niwapongeze Yanga na Sportpesa baada ya kudumu kama washirika kwa miaka nane. Mafanikio makubwa ya pande zote yametokana na ushirika huu ambao umekuwa na tija. Serikali inaendelea kutengeneza mazingira rafiki kwa wawekezaji ambayo wanayo dhamira ya kuingia kwenye mpira,” alisema

Rais wa Yanga Injinia Hersi Said ameipongeza SportPesa kwa kuendeleza uhusiano wake na Yanga ambao umeleta mapinduzi makubwa ya kiuchumi kwa mabingwa hao wa nchi

“Kabla ujio wa Sportpesa Yanga ilikwama. Licha ya ukubwa na ukongwe wake, Yanga ilishindwa kupata wachezaji wazuri, Yanga ilishindwa hata kusafiri bila changamoto. Lakini leo hii Yanga inagombea wachezaji wazuri na klabu kubwa Afrika."

"Mafanikio makubwa sana kutokana na udhamini mkubwa kutoka kwa Sportpesa. Tunawapongeza sana Sportpesa kwa namna ambavyo wamekuwa bega kwa bega na sisi,” alisema

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
5h ago
READ MORE →
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
8h ago
READ MORE →
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
10h ago
READ MORE →
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
12h ago
READ MORE →
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
14h ago
READ MORE →
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
15h ago
READ MORE →
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
15h ago
READ MORE →
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
17h ago
READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
20h ago
READ MORE →
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE →