Local,Normal News,Simba

Fadlu atabiri Simba imara msimu ujao

Joel JJ By Joel JJ
β€’
12 Aug 2025
Fadlu atabiri Simba imara msimu ujao

Kocha Mkuu wa Simba Fadlu Davids amesema kikosi chake kimeanza kuonyesha mabadiliko ya kiuchezaji baada ya wiki mbili za pre-season katika mji wa Ismailia, Misri

Jana Simba ilicheza mechi ya kirafiki dhidi ya timu inayoshiriki ligi kuu ya Misri, Kahraba Ismailia, mchezo uliomalizika kwa Mnyama kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 yaliyowekwa kambani na Mohamed Bajaber na Jonathan Sowah katika kila kipindi

Akizungumza baada ya mchezo huo, Fadlu alibainisha kuwa kikosi chake kimeonyesha mambo mengi mazuri baada ya muda mfupi wa mazoezi waliyofanya hapo Misri

"Tumecheza dhidi ya timu nzuri, mechi ilikuwa na ushindani, ukifanya tathmini tangu mechi yetu ya mwisho msimu uliopita na tulipo sasa, utaona tumepiga hatua"

"Ukiangalia kipindi cha kwanza ukitoa golikipa na wachezaji wengine wachache, tulianza na wachezaji wengi wapya lakini waliweza kucheza kwa kuzingatia mfumo wetu"

"Kipindi cha pili tulibadili timu nzima, ni mchezaji mmoja tu ambaye aliendelea kutoka kipindi cha kwanza, tuliendelea kucheza vizuri wachezaji waliongeza kasi na morali ya timu kwa ujumla"

"Ni mechi ambayo tungeweza kufunga mabao zaidi pengine matatu au manne, nimeridhika lakini bado hatujamaliza, tuna kazi ya kufanya kwenye uwanja wa mazoezi," alisema Fadlu

Kikosi cha Simba kitaendelea kujifua Ismailia kwa siku chache zaidi kabla ya kuelekea Cairo ambapo watacheza mechi zaidi ya kirafiki

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
2h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
6h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
9h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
12h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
12h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
12h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
14h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
18h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’