Kikosi cha Yanga leo kinatarajiwa kutua Rwanda tayari kwa mchezo wa Kimataifa wa kirafiki dhidi ya Rayon Sports ambao utapigwa Ijumaa, August 15 katika uwanja wa Amahoro
Baadhi ya maafisa wa Yanga wametangulia nchini humo kuweka sawa taratibu za mapokezi ya timu
Yanga imealikwa katika Tamasha la Rayon Day, tukio linalofanana na Wiki ya Mwananchi ambayo hufanywa na Yanga
Mechi hiyo itakuwa ya kwanza kwa kocha Romain Folz aliyetua Yanga mwezi uliopita akichukua mikoba iliyoachwa na Miloud Hamdi
Folz amekiandaa kikosi chake kwa takribani siku 10, ana matumaini makubwa ya kuanza vyema majukumu yake katika mchezo huo wa kirafiki
