Local,Transfer News,Simba

Simba yamalizana na kiungo kutoka Guinea

Joel JJ By Joel JJ
β€’
14 Aug 2025
Simba yamalizana na kiungo kutoka Guinea

Kocha Mkuu wa Simba Fadlu Davids ameridhishwa na kiwango cha kiungo Naby Camara raia wa Guinea na hivyo fundi huyo wa mpira anatarajiwa kupewa mkataba wa miaka miwili kuwatumikia Wekundu hao wa Msimbazi, imefahamika

Camara aliwasili Ismailia wiki iliyopita Fadlu akihitaji kumfuatilia mazoezini kabla ya kuidhinisha usajili wake

Nyota huyo aliyewahi kuitumikia CS Sfaxien, juzi alipata nafasi ya kucheza mchezo wake wa kwanza wa kirafiki wa kujipima nguvu dhidi ya Kahraba Ismailia, ikishinda kwa mabao 2-0 mabao yakifungwa na kiungo Mohammed Bajaber na mshambuliaji Jonathan Sowah.

Camara kwenye mchezo huo alipewa dakika 45 akionyesha kiwango kizuri, akicheza kama kiungo mkabaji kabla ya kubadilishwa na kupumzishwa. Camara pia anamudu kucheza nafasi ya beki wa kushoto na hata mlinzi wa kati

Fadlu amehitaji kuongeza nguvu eneo la kiungo mkabaji na beki wa kushoto, kumpata Camara ambaye anamudu kucheza nafasi zote mbili ni faida kwake

Aidha beki wa kushoto Hernest Malonga nae yuko Ismailia akisubiri hatma yake baada ya kujifua na kikosi cha Simba kwa takribani wiki moja

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
2h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
2h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
3h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
4h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
4h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
5h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
19h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
19h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
20h ago
READ MORE β†’