Local,Normal News,Yanga

Yanga yatua Rwanda kuikabili Rayon, yapokelewa kwa shangwe

Joel JJ By Joel JJ
β€’
14 Aug 2025
Yanga yatua Rwanda kuikabili Rayon, yapokelewa kwa shangwe

Yanga tayari iko Rwanda kwa ajili ya mchezo wa kirafiki dhidi ya Rayon Sports ambao utapigwa kesho Ijumaa katika uwanja wa Amahoro. Huu utakuwa mchezo wa kwanza kwa Kocha Mkuu wa mabingwa hao wa Tanzania Romain Folz

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga Ali Kamwe amesema licha ya muda mfupi ambao kocha huo amepata kukiandaa kikosi, wachezaji wako tayari kupambana na kuwapa furaha mashabiki wao

Kamwe amesema Yanga imepata mapokezi makubwa Kigali ambayo yamemshangaza Folz na baadhi ya wachezaji wapya waliojiunga na timu hiyo katika dirisha hili

"Timu ilipowasili uwanja wa ndege tulipata mapokezi makubwa ambayo yalimshangaza kocha wetu Romain Folz na hata nyota wapya. Mapokezi haya ulikuwa ujumbe mahsusi kwao kuwaonyesha Yanga ni kubwa kiasi gani"

"Naweza kusema kazi kubwa iliyofanyika katika maandalizi kuelekea mchezo dhidi ya Rayon ilikuwa kujenga utimamu wa mwili. Maandalizi ya kimbinu yalifanyika kwa asilimia 25. Lakini wachezaji wetu wako tayari kupambana na kuwapa furaha mashabiki wetu hapa Rwanda na huko nyumbani Tanzania," alisema Kamwe

Akizungumzia mipango ya pre-season baada ya mchezo huo, Kamwe amesema kikosi cha Yanga kitarejea jijini Dar es salaam kukamilisha maandalizi yake

"Mpaka sasa sijapewa taarifa kama timu itasafiri nje ya nchi kuendelea na pre-season hivyo baada ya mchezo dhidi ya Rayon tutarejea nyumbani (Tanzania) kuendelea na maandalizi yetu," aliongeza Kamwe

Awali kulikuwa tetesi kuwa Yanga ingesafiri nje ya nchi kukamilisha wiki mbili nyingine za pre-season. Lakini ni wazi kwa muda uliobaki, uamuzi wa kukamilisha pre-season Tanzania ni bora zaidi

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
8h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
11h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
13h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
15h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
17h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
18h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
18h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
20h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
23h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’