Yanga wamkumbuka Mzee Katundu

Joel JJ By Joel JJ β€’ 26th August 2025


Yanga wamkumbuka Mzee Katundu

Leo imekuwa siku ya kipekee kwa familia kubwa ya Yanga SC, baada ya Rais wa Klabu, Injinia Hersi Said, kumtembelea Katibu wa zamani wa Yanga, Mzee Jabir Katundu, na kumkabidhi zawadi za jezi mpya za msimu wa 2025/26.

Mzee Katundu, ambaye aliwahi kuhudumu kama Katibu wa Klabu kati ya mwaka 1962 hadi 1966, alihudumu chini ya Uenyekiti wa marehemu Mohamed Mabosti. Kipindi chake cha uongozi kilikuwa cha kihistoria, kwani kilisaidia kuimarisha msingi wa Yanga na kuiweka kwenye ramani ya soka la Tanzania na Afrika Mashariki.

Katika ziara hiyo, Rais Hersi Said alikabidhi kwa heshima kubwa jezi zote tatu za matoleo mapya ya msimu huu, huku akimuelezea Mzee Katundu dhamira na maudhui yaliyopelekea ubunifu wa jezi hizo.

Kila jezi inabeba simulizi na alama ya heshima kwa historia na mafanikio ya klabu, zikionyesha mshikamano kati ya vizazi vilivyopita na kizazi cha sasa.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.