International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Jumatano August 27 2025

Joel JJ By Joel JJ
β€’
27 Aug 2025
Tetesi za usajili Ulaya, Jumatano August 27 2025

Mshambuliaji wa Sweden Alexander Isak, mwenye umri wa miaka 25, ameiambia Newcastle kwamba bado anataka kuondoka na kujiunga na Liverpool licha ya jitihada za mwenyekiti wa klabu Yasir Al-Rumayyan na kikao na mmoja wa wamiliki wenza Jamie Reuben. (Telegraph)

Manchester United imefikia makubaliano ya awali na Real Betis kwa ajili ya winga wa Kibrazili Antony, 25, kurejea katika klabu hiyo ya Hispania kwa mkopo wenye sharti la kununuliwa moja kwa moja. (Telegraph)

Manchester United pia inatarajia kukubaliana masharti binafsi na kipa Senne Lammens ili kumsajili mchezaji huyo wa Ubelgiji mwenye umri wa miaka 23 kutoka Royal Antwerp kabla ya dirisha la usajili kufungwa. (Telegraph)

Real Madrid na Atletico Madrid wanamfuatilia kiungo wa timu ya taifa ya Uingereza Kobbie Mainoo, 20, wa Manchester United ambaye anataka kuondoka baada ya kukosa nafasi kwenye kikosi cha Old Trafford. (Mail)

Mainoo pia anasakwa Fulham, sambamba na winga wa Kiingereza wa Arsenal Reiss Nelson, 25. (Teamtalk)

Porto wako karibu kufikia makubaliano ya mkopo yenye sharti la kumnunua moja kwa moja beki wa Poland Jakub Kiwior, 25, wa Arsenal. (Sky Sports)

Crystal Palace wanajiandaa kwa mazungumzo na Liverpool kuhusu kiungo mshambuliaji Mwingereza Harvey Elliott, 22, wakiharakisha mipango ya kumpata mrithi wa Eberechi Eze, 27, ambaye amejiunga na Arsenal. (Football Insider)

Brentford wanamfikiria mshambuliaji wa Ujerumani Max Beier, 22, wa Borussia Dortmund, huku klabu hiyo ya Bundesliga ikiwa karibu pia kukamilisha dili la kumsaini mshambuliaji wa Ureno Fabio Silva, 23, kutoka Wolves. (Sky Sports)

Roma wamefanya mazungumzo na Chelsea pamoja na wawakilishi wa Tyrique George kuhusu kumsaini winga huyo wa Kiingereza mwenye umri wa miaka 19. (Gianluca di Marzio)

Alejandro Garnacho amekataa ofa mpya kutoka klabu moja ya Saudi Pro League katika saa 48 zilizopita huku mazungumzo kati ya Manchester United na Chelsea kuhusu winga huyo wa Argentina mwenye umri wa miaka 21 yakiwa yamefikia hatua za mwisho. (Fabrizio Romano)

Bayer Leverkusen na Galatasaray wako tayari kushindana na Crystal Palace kumsajili beki wa Manchester City na timu ya taifa ya Uswizi Manuel Akanji, 30. (Independent)

West Ham wako karibu kukamilisha dili la paundi milioni 17.3 kumsajili kiungo wa Kifaransa Soungoutou Magassa, 21, kutoka AS Monaco. (Guardian)

Dili la mkopo kwa kiungo mkabaji wa Ivory Coast Ibrahim Sangare, 27, wa Nottingham Forest pia linafuatiliwa na West Ham, ambao pia wanavutiwa na kiungo wa Mfaransa Junior Mwanga, 22, wa Strasbourg na kiungo Mwingereza Hayden Hackney, 23, wa Middlesbrough. (Sky Sports)

Nottingham Forest wamekataliwa ofa ya awali ya karibu paundi milioni 10 kwa ajili ya beki wa kulia Muitaliano Nicolo Savona, 22, kutoka Juventus. (Gianluca di Marzio)

Crystal Palace wamefikia makubaliano ya awali na Villarreal kwa ajili ya kiungo wa Kihispania Yeremy Pino, 22, kwa dau linaloweza kufikia paundi milioni 26. (AS)

Kiungo wa Liverpool James McConnell, 20, anatarajiwa kujiunga na Ajax kwa mkopo kwa msimu wa 2025-26 baada ya nyota huyo wa kimataifa huyo wa England chini ya miaka 20 kusaini mkataba mpya wa miaka mitano na klabu hiyo. (Athletic)

BBC

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
7h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
10h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
12h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
14h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
16h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
17h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
17h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
19h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
22h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’