Local,Normal News,Simba

Fadlu ataka mshambuliaji mwingine Simba

Joel JJ By Joel JJ
β€’
27 Aug 2025
Fadlu ataka mshambuliaji mwingine Simba

Kocha Mkuu wa Simba Fadlu Davids ameeleza kuridhishwa na mwenendo wa kikosi chake baada ya wiki nne za pre-season huko Misri

Leo Simba inakamilisha mechi ya mwisho ya kirafiki dhidi ya FS Fassel ya Liberia kabla ya kurejea Tanzania siku ya kesho Alhamisi

Akizungumza jana baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Wadi Degla, Fadlu alibainisha kuhitaji kuongezewa mshambuliaji mwingine ambaye ataendana na ushindani wa mechi kubwa za maamuzi

"Niwe tu muwazi bado nahitaji mchezaji mmoja mwenye X Factor kwenye eneo la ushambuluaji, najua tumepata sapoti kubwa sana kutoka kwa Rais Mo Dewji na mchango wake msimu huu umekuwa mkubwa Sana"

"Natumai sasa tunapoelekea mwishoni mwa usajili Jayrutty anaweza kutusaidia kumpata mchezaji huyo mmoja mkubwa ambaye anaweza kutupa utofauti kwenye eneo la mwisho"

"Unakumbuka baadhi ya mechi ngumu msimu uliopita tulikuwa tunakosa mchezaji mkubwa ambaye anaweza kukupa hizo x Factor, mechi kama ya fainali ya CAF CC na hata mechi ya mwisho wa msimu dhidi ya Yanga tulikuwa tunakosa mchezaji kama huyo"

"Tunahitaji kufanya vyema kwenye ligi ya ndani lakini pia tunakazi kubwa ya kufanya kimataifa,” alisema Fadlu katika mahojiano ya Azam TV

Simba imerejesha nchini mshambuliaji Seleman Mwalimu aliyekuwa akiitumikia Wydad CA, inaelezwa tayari usajili wake umekamilika na atajiunga na kikosi jijini Dar es salaam

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
46m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’