International,Normal News,Simba

Simba yamshusha Mwalimu Dar

Joel JJ By Joel JJ
β€’
28 Aug 2025
Simba yamshusha Mwalimu Dar

Klabu ya Simba imethibitisha kumsajili mshambuliaji Suleiman Mwalimu Gomez kutoka Wydad Athletic

Mwalimu aliyezitumikia Singida BS/Fountain Gate kabla ya kutimkia Wydad, anarudi Tanzania kwa mkopo wa msimu mzima Simba ikiwa na nafasi ya kumsajili moja kwa moja pale muda wa mkopo utakapomalizika

Ni usajili uliokuwa ukisubiri uthibitisho tu kwani Simba ilikamilisha usajili wake tangu wiki iliyopita na alitua nchini juzi tayari kuungana na waajiri wake wapya

Mwalimu aliitumikia Wydad katika michuano ya kombe la Dunia la klabu mwezi Juni akipata nafasi katika mechi zote tatu mojawapo ikiwa dhidi ya Manchester City

Kuelekea msimu ujao safu ya ushambuliaji ya Simba sasa itaongozwa na Jonathan Sowah, Mwalimu na Steven Mukwala baada ya Lionel Ateba kuuzwa

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’