International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Alhamisi August 28 2025

Joel JJ By Joel JJ
β€’
28 Aug 2025
Tetesi za usajili Ulaya, Alhamisi August 28 2025

Manchester United wako karibu kufikia makubaliano ya dau kati ya pauni milioni 35 na 40 kumuuza winga wa Argentina mwenye umri wa miaka 21 Alejandro Garnacho kwenda Chelsea ya Ligi Kuu England (Telegraph)

AC Milan wameingia katika mbio za kumsajili mshambuliaji wa Chelsea Christopher Nkunku huku mfaransa huyo mwenye umri wa miaka 27 pia akiwaniwa na Bayern Munich mabingwa wa Bundesliga na klabu yake ya zamani RB Leipzig (Athletic)

Newcastle wanatarajiwa kuwasilisha ofa mpya ya pauni milioni 60 kwa mshambuliaji wa Norway mwenye miaka 25 Jorgen Strand Larsen baada ya awali Wolves kukataa madau mawili ya pauni milioni 50 na 55 awali (Sky Sports)

Kipa wa Paris St-Germain Gianluigi Donnarumma bado hajaondoa matumaini ya kuondoka kabla ya dirisha kufungwa huku Manchester City ikionekana kuwa chaguo bora zaidi endapo kipa wa Brazil Ederson ataondoka klabuni hapo (Sky Sports)

Hakuna mazungumzo yanayoendelea kati ya Al-Nassr ya Saudi Arabia na Manchester City kuhusu Ederson lakini Galatasaray bado wana hamu ya kumsajili kipa huyo mwenye miaka 32 (Fabrizio Romano)

West Ham wanamuwinda kipa wa Brazil mwenye miaka 29 John Victor kutoka Botafogo lakini klabu hiyo inataka dau kubwa zaidi ya pauni milioni 6 endapo uhamisho huo utakuwa wa kudumu (Sky Sports)

West Ham wameijulisha Everton kuwa wanataka kumbakisha kiungo wao wa Czech mwenye miaka 30 Tomas Soucek baada ya klabu hiyo ya Merseyside kuonyesha nia ya kumsajili (Athletic)

Tottenham wamekubaliana kumpeleka beki wa Croatia mwenye miaka 18 Luka Vuskovic kwa mkopo wa msimu mzima Hamburg huku kocha Thomas Frank akitafuta kuongeza chaguo jingine kwenye safu ya ulinzi (Standard)

Sunderland wanatarajia kumbembeleza beki wa West Ham na Morocco Nayef Aguerd mwenye miaka 29 ajiunge nao lakini Marseille AC Milan na AS Roma pia wanavutiwa naye (Footmercato)

Manchester City wameijulisha Tottenham kwamba hawana mpango wa kumruhusu winga wa Brazil mwenye miaka 21 Savinho kuondoka msimu huu wa joto hata kama itatolewa ofa zaidi ya pauni milioni 60 (Fabrizio Romano)

Sunderland pia imewasilisha ofa mpya ya pauni milioni 24 kwa Bologna kwa ajili ya beki wa Colombia mwenye miaka 27 Jhon Lucumi (Sky Sports)

Genoa wanamfikiria Maxwel Cornet wa West Ham baada ya mchezaji huyo wa Ivory Coast kumvutia kocha Patrick Vieira akiwa kwa mkopo msimu uliopita (Tuttomercatoweb)

Kiungo mshambuliaji wa Bournemouth na Ivory Coast mwenye miaka 25 Hamed Traore anatarajiwa kujiunga na Marseille kwa mkopo wenye kipengele cha kumnunua moja kwa moja (Footmercato)

Wolves wanavutiwa na mshambuliaji wa Genk Tolu Arokodare mwenye miaka 24 mshambuliaji wa Nigeria aliyemaliza msimu uliopita akiwa mfungaji bora wa ligi ya Ubelgiji kwa mabao 17 (Sky Sports)

BBC

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
6h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
10h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
11h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
13h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
16h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
16h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
16h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
18h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
22h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’