Kamwe aiomba dabi Wiki ya Mwananchi

Joel JJ By Joel JJ β€’ 28th August 2025


Kamwe aiomba dabi Wiki ya Mwananchi

Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Yanga Ali Kamwe amesema mchezo wa Ngao ya Jamii kati ya Yanga dhidi ya Simba una umuhimu wa kipekee kwani fedha zitakazopatikana zitakwenda kusaidia yatima na wale wenye uhitaji

Kamwe amesema mchezo huo unapaswa kupigwa kama ulivyopangwa Septemba 16 lakini kama kuna ulazima wa kuchezwa mapema Yanga iko tayari mchezo huo kupigwa siku ya kilele cha wiki ya Mwananchi Septemba 12

Kumekuwa na sintofahamu kuhusu mchezo huo zikiibuka taarifa kuwa klabu ya Simba imeomba usogezwe mbele kwa kuwa Septemba 20 wanakabiliwa na mchezo wa ligi ya mabingwa hatua ya awali nchini Botswana

Kamwe amebainisha kuwa Yanga haina tatizo na tarehe ya mchezo huo na wako tayari kucheza lakini kama italazimu, urudishwe nyuma Septemba 12 ili kuondoa 'kipengele'

"Mchezo wa Ngao ya Jamii una umuhimu mkubwa sana kwani mapato yatakayopatikana yanakwenda kusaidia Jamii hivyo sisi (Yanga) tuko tayari kucheza katika tarehe hiyo iliyopangwa"

"Lakini nimesikia wenzetu wameomba usogezwe mbele kutokana na ratiba yao ya ligi ya mabingwa, kwa maoni yangu naona mchezo upigwe kama ulivyopangwa"

"Hata sisi tuna mchezo Angola lakini naamini muda uliopo utatosha kwa timu kusafiri na kukamilisha maandalizi kwani Angola na Botswana sio mbali ni mwendo wa saa chache tu"

"Lakini kama haiwezekani, sisi tuna mchezo wa wiki ya Mwananchi Septemba 12 na tutacheza dhidi ya Bandari Fc. Tuko tayari kuwa 'stopisha' Bandari Fc ili mchezo upigwe siku hiyo," alisema Kamwe


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.