Morocco ataka uzalendo kwa Stars

Joel JJ By Joel JJ • 1st September 2025


Morocco ataka uzalendo kwa Stars

Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa Tanzania (Taifa Stars), Hemed Suleiman Morocco, ameshauri waandishi wa habari nchini kuonesha uzalendo kwa kujitokeza kwa wingi kwenye mikutano na shughuli za Timu ya Taifa.

Akizungumza wakati wa kutangaza kikosi cha kitakachoingia kambini Septemba 2, 2025 kwaajili ya maandalizi ya mechi mbili za kufuzu kombe la dunia 2026, Suleiman amesema ni jambo la kusikitisha kuona mwitikio mdogo wa vyombo vya habari, tofauti na nchi nyingine ambapo waandishi hujitokeza kwa wingi kuunga mkono timu zao.

“Waandishi wanapaswa kuisapoti timu yao. Hata wakitusema sisi tunachukulia kama changamoto, ila uwepo wao ni muhimu kama ishara ya uzalendo,” alisema Morocco.

Kocha huyo ameongeza kuwa mwitikio mkubwa wa waandishi unaweza kuongeza motisha kwa wachezaji na benchi la ufundi kuelekea mechi za kimataifa.

Morocco alitangaza kikosi cha wachezaji 23 ambao wataiwakilisha Tanzania katika mechi mbili za kuwania kufuzu kombe la Dunia dhidi ya Congo na Niger


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.