International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Jumatatu Septemba 08 2025

Joel JJ By Joel JJ
β€’
8 Sep 2025
Tetesi za usajili Ulaya, Jumatatu Septemba 08 2025

Klabu ya Liverpool haitamsajili beki wa Crystal Palace Marc Guehi mwezi Januari. The Reds walishindwa kupata pauni milioni 35 za kumsajili mchezaji huyo wa kimataifa wa Uingereza mwenye umri wa miaka 25 wiki iliyopita. Mkataba wake utakapokamilika msimu ujao wa kiangazi. (Times - usajili unahitajika)

Majadiliano kati ya mlinzi wa Liverpool na Ufaransa Ibrahima Konate kuhusu kandarasi mpya bado yanaendelea na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 ambaye anaongoza orodha ya wachezaji wanaolengwa na Real Madrid. (Fabrizio Romano via Givemesport)

Mshambuliaji wa Ufaransa Kylian Mbappe, 26, amemuomba Mohamed Salah wa Liverpool kuungana naye Real Madrid. Winga huyo wa Misri, 33, alitia saini mkataba mpya wa miaka miwili Anfield mwezi Aprili lakini huenda akaingiwa na tamaa ya kuhamia Bernabeu. (Teamtalk)

Kipa wa Manchester United Andre Onana amekubali kujiunga na klabu ya Uturuki Trabzonspor kwa mkopo lakini klabu hiyo haikupewa chagua la kumnunua mchezaji huyo wa kimataifa wa Cameroon mwenye umri wa miaka 29 katika mkataba huo. (Fabrizio Romano)

Onana ameongeza mshahara wake maradufu kwa kukubali kujiunga na Trabzonspor kutoka Manchester United kwa msimu uliosalia. (Mail)

Klabu za Aston Villa, Leeds United na Newcastle United zinavutiwa na mshambuliaji wa Crystal Palace Mfaransa Jean-Philippe Mateta, 28 na huenda zikawania kumsjili Januari. (Caught Offside)

Klabu za Birmingham City, Wrexham na West Brom zina nia ya kumsajili kiungo wa wa Uingereza Dele Alli kwa uhamisho wa bure. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29 hivi majuzi alikatisha mkataba wake na klabu ya Italia ya Como. (Mail)

Kipa wa Lazio Christos Mandas, 23, anatarajiwa kuamua mustakabali wake mwezi Januari baada ya kupoteza nafasi yake kwenye kikosi cha kwanza, huku Wolves wakitarajiwa kufufua nia yao, baada ya kuwasilisha ombi la pauni milioni 17.3 kwa mchezaji huyo wa kimataifa wa Ugiriki msimu wa kiangazi. (Corriere dello Sport)

Beki wa Inter Milan Denzel Dumfries amesema angefurahia fursa ya kucheza Ligi ya Premia baada ya majira ya kiangazi ambapo mchezaji huyo wa kimataifa wa Uholanzi, 29, alihusishwa na Manchester United. (Metro)

BBC

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
7m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
36m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’