Local,Normal News,

Thamani ya Yanga ni Bilioni 100

Joel JJ By Joel JJ
โ€ข
8 Sep 2025
Thamani ya Yanga ni Bilioni 100

Klabu ya Yanga ina thamani ya Shilingi Bilioni 100, baada ya kamati maalum iliyoundwa kwa ajili ya tathmini hiyo kukamilisha kazi yake.

Akizungumza jana katika Mkutano Mkuu wa Wanachama uliofanyika kwenye ukumbi wa SuperDome, Masaki jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Alex Mgongolwa, alisema tathmini hiyo imefanywa na kampuni ya kimataifa ya ushauri wa uwekezaji na mali isiyohamishika, Colliers International.

Mgongolwa alisema hatua hiyo ni mwanzo wa mchakato mpana wa klabu kuingia katika mfumo wa kisasa wa uendeshaji kwa kuuza hisa, na kuongeza kuwa thamani hiyo itatumika kama mwongozo katika taratibu zote za uwekezaji zitakazoanza hivi karibuni.

Aidha, katika Mkutano huo wa Wanachama, ilisomwa taarifa ya mapato na matumizi kwa msimu uliopita 2024/25 naย ikasomwa bejeti ya klabu kwa msimu ujao 2025/26

Akisoma taarifa ya mapato na matumizi ya klabu, Makamu wa Rais wa Yanga Arafat Haji alisema mapato ya klabu kwa msimu uliopita ni Tsh Bilioni 25.6 huku matumizi yakiwa Tsh Bilioni 25.3 kukiwa akiba ya takribani laki 3

Aidha Bajeti ya Yanga kwa msimu ujao 2025/26 ni Tsh Bilioni 33.6

More Stories

Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
4m ago
READ MORE โ†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
33m ago
READ MORE โ†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE โ†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE โ†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE โ†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE โ†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE โ†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE โ†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE โ†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE โ†’