Local,Normal News,

Beki mpya Simba apagawisha mashabiki

Joel JJ By Joel JJ
β€’
12 Sep 2025
Beki mpya Simba apagawisha mashabiki

Wakati Simba ikichuana na Gor Mahia jana katika mchezo wa kirafiki maalum kuhitimisha Tamasha la Simba Day, mashabiki wa Simba walikuwa makini kuangalia viwango vya nyota wapya waliosajiliwa katika dirisha hili

Kwa ujumla Wanasimba walionekana kuridhishwa na viwango vilivyoonyeshwa na wachezaji wote wapya waliopewa nafasi katika mchezo huo ambao Simba iliibuka na ushindi wa mabao 2-0 hasa ikizingatiwa ulikuwa mchezo wa kwanza kuwashuhudia nyota hao

Lakini wapo wachezaji miongoni mwao ambao waliacha tabasamu kwa mashabiki kwa kile walichoonyesha katika mchezo huo

Beki kisiki Rushine De Reuck aliyetua Simba kutoka klabu ya Mamelodi Sundowns ni miongoni mwa wachezaji hao

Kama ni kupewa alama kulingana na kazi aliyofanya uwanjani, basi De Reuck angeweza kuondoka na alama 9 kati ya 10

Mahiri katika kupiga pasi, katika pasi 80 alizopiga, 78 zilifika kwa usahihi. De Reuck alicheza mipira ya hatari 10 huku akifanikiwa kupiga mipira mirefu 4 iliyofika

De Reuck alionyesha umahiri wake katika kuzima mashambulizi na kuanzisha mipira kwa pasi zake zilizonyooka mithiri ya rula

Ni wazi ujio wake unakwenda kuimarisha eneo la safu ya ulinzi na pengine huenda akawa beki tegemeo katika eneo hilo akishirikiana na Abdulrazak Hamza na Carabou Chamou huku pia Wilson Nangu na Masinde wakitarajiwa kuwapa changamoto mabeki hao

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
46m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’