Local,Normal News,Yanga

Yanga kuanza kampeni ya kutetea ubingwa kwa Mkapa

Joel JJ By Joel JJ
β€’
22 Sep 2025
Yanga kuanza kampeni ya kutetea ubingwa kwa Mkapa

Kikosi cha Yanga leo kinarejea mazoezini kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wa ligi kuu dhidi ya Pamba Jiji ambao utapigwa Jumatano, Septemba 24 katika uwanja wa Benjamin Mkapa

Msimu huu Yanga imechagua kutumia dimba la Mkapa kama uwanja wake wa nyumbani katika mechi za ligi kuu, kombe la CRDB na Ligi ya mabingwa

Ni baada ya Serikali kufungua uwanja huo ambao kwa takribani misimu miwili haukutumika kwa mechi za ligi kutokana na ukarabati uliokuwa ukiendelea

Mabingwa hao wa ligi kuu kwa misimu minne mfululizo, wataanza kulisaka taji la tano mtawalia katika mchezo huo ambao utapigwa saa 1 usiku

Yanga kurejea dimba la Mkapa ni habari njema kwa mashabiki ambao sasa watapata nafasi ya kuishuhudia timu yao kwa wingi

Katika misimu miwili iliyopita, Yanga ilitumia viwanja vya Azam Complex na KMC Complex ambavyo vilichukua idadi ndogo ya mashabiki wasiozidi 7000

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
2h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’