Kocha Mkuu wa Yanga Romain Folz amesema ana imani na mshambuliaji Prince Dube licha ya kukosa nafasi nyingi katika mchezo wa mkondo wa kwanza hatua ya awali ligi ya mabingwa dhidi ya Wiliete SC
Kesho Jumamosi Yanga itakuwa mwenyeji wa Wiliete SC katika uwanja wa Benjamin Mkapa ikiwa kifua mbele kufuatia ushindi wa mabao 3-0 katika mchezo wa kwanza uliopigwa Angola





