Local,Normal News,Simba

Kocha Simba aanza na safu ya ulinzi

Joel JJ By Joel JJ
β€’
15 Oct 2025
Kocha Simba aanza na safu ya ulinzi

Baada ya kuruhusu mabao matano katika mechi mbili za kirafiki, mkufunzi wa Simba Dimitar Pentev ameweka wazi mpango mkakati wake wa kuboresha eneo la ulinzi

Simba licheza mechi mbili za kirafiki dhidi ya Al Hilal ambapo mechi ya kwanza iliibuka na ushindi wa mabao 2-1 na mechi ya pili wekundu hao wa Msimbazi wakakubali kupoteza kwa mabao 4-1

Katika mazoezi yanayoendelea Mo Simba Arena, Pentev ameoneka kuweka mkazo na kutoa maelekezo mengi vile anataka wachezaji wacheze pale timu inapokuwa haina mpira

Kocha huyo raia wa Bulgaria anapendelea mfumo wa 4-3-3 huku akiwataka wachezaji wake kucheza pamoja wakiwa na mpira na hata bila mpira 'tatal football'

Pentev amesema mechi dhidi ya Al Hilal zimempa mwanga wa nini anapaswa kuboresha na pia wachezaji gani wanaweza kuendana na mbinu zake

"Tunahitaji kuwa na timu inayocheza kwa mpangilio, inayoshambulia kwa hesabu na kujilinda kwa pamoja, mechi hizi zimeniwezesha kuona nani yuko tayari kupigania nembo ya Simba, nadhani kila kitu kitakaa sawa, " alisema Pentev

Simba inakamilisha maandalizi yake leo kabla ya kusafiri kuelekea Eswatin siku ya kesho Alhamisi kuikabili Nsingizini Hotspurs kuwania tiketi ya kufuzu hatua ya makundi ligi ya mabingwa barani Afrika

Mechi ya mkondo wa kwanza itapigwa Jumapili Oktoba 19 na marudiano kupigwa wiki moja baadae jijini Dar es salaam

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
2h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’