Local,Normal News,Yanga

Mashabiki wa Yanga kupeleka shangwe Malawi

Joel JJ By Joel JJ
β€’
15 Oct 2025
Mashabiki wa Yanga kupeleka shangwe Malawi

Jumamosi Oktoba 18 katika uwanja wa Bingu, Yanga itakuwa ugenini kuikabili Silver Strikers katika mchezo wa mkondo wa kwanza kuwania tiketi ya kutinga hatua ya makundi ligi ya mabingwa barani Afrika

Habari njema ni kuwa Wananchi wana uhakika wa sapoti kubwa kutoka kwa mashabiki wao kwani licha ya wale wanaoishi nchini Malawi, kuna msafara utaondoka leo kuelekea Malawi kuongeza hamasa katika mchezo huo

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga Ali Kamwe amesema zaidi ya mabasi 40 yataondoka leo kulekea Malawi

"Msafara wa wanachama na mashabiki utaondoka Jumatano (leo) ambapo mpaka sasa tuna uthibitisho wa zaidi ya mabasi 40 kuelekea Malawi"

"Viongozi na wachezaji wao wataondoka siku ya Alhamisi ambapo timu ikifika Malawi tutakuwa na 'session' mbili au tatu za mazoezi kuelekea siku ya mchezo ambayo ni Jumamosi," alisema Kamwe

Yanga imepania kufuzu hatua ya makundi ya ligi ya mabingwa kwa msimu wa tatu mfululizo. Wananchi wanahitaji kuanza vyema ugenini kabla ya mechi ya pili itakayopigwa jijini Dar es salaam Oktoba 25

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’