Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limevifungia viwanja wa Liti, Singida na Sokoine, Mbeya kutumika kwa michezo ya Ligi kwa kukosa vigezo vya kikanuni na sheria za mpira wa miguu.
Katika Taarifa iliyotolewa na Shirikisho hilo imeeleza kuwa miundombinu ya viwanja hivyo haikidhi matakwa ya Kanuni kama ilivyoainishwa kwenye masharti ya Kanuni ya Leseni za Klabu
Kufuatia uamuzi huo, timu zinazotumia viwanja hivyo kwa michezo yao ya nyumbani zitalazimika kutumia uwanja mwingine kama Kanuni inavyoelekeza mpaka pale vitakapofunguliwa, baada ya kufanyiwa marekebisho na kukaguliwa na TFF.
Aidha, TFF inazikumbusha Klabu zote kuendelea kutunza na kuboresha miundombinu ya viwanja.



