Local,Normal News,Yanga

Folz aweka mkakati wa ushindi Malawi

Joel JJ By Joel JJ
β€’
15 Oct 2025
Folz aweka mkakati wa ushindi Malawi

Kocha Mkuu wa Yanga Romain Folz amesema amekiandaa kikosi chake kwenda kupambana huko Malawi ili kuhakikisha wanaanza vyema mechi ya mkondo wa kwanza kuwania kutnga hatua ya makundi ya michuano ya ligi ya mabingwa (CAFCL) dhidi ya Silver Strikers

Yanga inatarajiwa kuondoka nchini kesho Alhamisi kuelekea Malawi ambapo mchezo huo utapigwa siku ya Jumamosi, Oktoba 18

Akizungumzia maandalizi ya kikosi chake, Folz amesema hakuna mechi nyepesi katika michuano ya ligi ya mabingwa hivyo wamejipanga kukabiliana na timu ngumu kama ilivyokuwa mchezo uliopita dhidi ya Wiliete Sc

"Tumekuwa na maandalizi mazuri pamoja na kuwa katika kipindi hiki cha mapumziko ya FIFA tumewakosa baadhi ya wachezaji lakini niseme tumepata wakati mzuri wa kujiandaa na tuko tayari kukabiliana na mpinzani anayekuja mbele yetu"

"Hii ni ligi ya mabingwa hivyo hatutarajii mechi nyepesi kama ilivyokuwa mechi iliyopita dhidi ya Wiliete Sc. Tumepata muda wa kuwafuatilia Silver Strikers, ni timu nzuri tunajua ni mkakati gani tunapaswa kwenda nao Malawi"

"Muhimu kabla ya kufikiria nini tunakwenda kufanya, jambo la kwanza ni kumuheshimu mpinzani na kuwa tayari kukabiliana nae huku tukiweka malengo ya kushinda," alisema Folz

Folz amesisitiza kuwa timu yake itaendelea kuwa na mabadiliko na kuimarika siku hadi siku jambo muhimu akiwataka mashabiki kuwa na imani juu ya kazi inayofanywa na benchi la ufundi

"Kama nilivyosema mwanzo, hii sio kazi ya siku moja, nafurahi kuona tunaendelea kuimarika na naamini tutaendelea kuwa bora siku hadi siku"

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
2h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
2h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
3h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
4h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
4h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
5h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
19h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
19h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
20h ago
READ MORE β†’