Mikiki mikiki ya ligi kuu ya NBC inaendelea leo Ijumaa kwa mechi mbili kupigwa baada ya mapumziko ya kalenda ya FIFA
Pamba Jiji watakuwa wenyeji wa Mashujaa Fc katika mchezo utakaopigwa saa 8 mchana wakati Fountain Gate wakiwakaribisha Dodoma Jiji katika mchezo utakaopigwa saa 10 jioni
Mechi nyingine kati ya KMC dhidi ya Mbeya City itapigwa kesho Jumamosi saa 10 jioni




