Kiungo mshambuliaji Allan Okello ameanza rasmi kujifua na kikosi cha Yanga siku chache tangu ajiunge na mabingwa hao wa nchi.
Yanga imemsajili Okello kutoka klabu ya Vipers Fc ya Uganda, akisaini mkataba wa miaka miwili na nusu.
Yanga inatarajiwa kumtumia nyota huyo kwenye michuano ya ligi ya mabingwa, Yanga ikitarajiwa kuumana na Al Ahly Januari 23.











