Local,International,Normal News,

Mane, Pape Thiaw ni mashujaa Senegal

Joel JJ By Joel JJ
β€’
21 Jan 2026
Mane, Pape Thiaw ni mashujaa Senegal

Fainali za Kombe la Mataifa Afrika (AFCON) zimetamatika juzi kwa taifa la Senegal kuibuka mshindi kwa kuibwaga mwenyeji, Morocco kwa mabao 1-0.

Mjadala uliobaki masikioni na machoni mwa wapenda mpira Afrika na duniani ni nani anayepaswa kuwa shujaa wa michezo huo ambao licha ya kutoa bingwa lakini ulikumbwa na vurugu.

Je? ni Sadio Mane au kocha wake Pape Thiaw ambaye anapaswa kupewa pongezi, huku mmoja akihamasisha wenzake kurejea uwanjani baada ya kutokea vurugu na mwingine akihamasisha wachezaji kuondoka uwanjani.

Tukio kuu katika fainali hiyo litakalosalia katika kumbukumbu ya historia ya michuano hiyo ni katika dakika ya 98 pale Senegal walipotoka uwanjani na kususia mechi hiyo kwa muda wa dakika 17.

Chanzo kikiwa ni uamuzi wa refa Jacques Ndala aliyewapa Morocco penalti baada ya kutumia uamuzi wa VAR. Malick Diouf wa Senegal alidaiwa kumchezea rafu mshambulaiji wa Morocco, Brahim Diaz.

Hatua hiyo ilimlazimu kocha wa Senegal Pape Thiew kuwahamasisha wachezaji wake kutoka kabisa uwanjani akilalamika kuwa wamedhulumiwa.

Mchezaji aliyebaki uwanjani ni Sadio Mane tu, nahodha wa Senegal aliyewashauri wenzake kurejea, na baada ya dakika 17 walirejea na kukubali kuendelea na mchezo.

Kwa bahati nzuri kwa Senegal, Brahim Diaz aliyefunga mabao matano kwenye michuano hiyo, aliipiga penalti hiyo iliyonyakwa na kipa Eduad Mendy wa Senegal.

Baada ya kutamatika ziliongezwa dakika za ziada 30 ndipo Senegal ikaibuka mshindi kwa bao 1-0 lililofungwa na nyota wao Pape Gueye na kuwafanya kunyakua kombe hilo.

Je? kati ya wawili hao nani anapaswa kupewa pongezi, kocha aliyehamasisha wachezi kuondoka uwanjani ambapo walitii amri hiyo na baadaye Sadio Mane kuwafuata na kuwahamasisha kurudi na kuendelea na mchezo ambao baadaye waliibuka na ushindi.

IPP Media

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’