Local,Normal News,Yanga

Kocha Yanga apania kuiduwaza Al Ahly CAFCL

Joel JJ By Joel JJ
21 Jan 2026
Kocha Yanga apania kuiduwaza Al Ahly CAFCL

Kocha Mkuu wa Yanga Pedro Goncalves amesema wachezaji wake wana morali kubwa kuelekea mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Al Ahly ambao utapigwa Ijumaa, Januari 23 huko Misri.

Akizungumza na wanahabari mapema leo muda mfupi kabla ya kuondoka nchini, Goncalves alisema licha ya kukabiliwa na safari ndefu lakini wanakwenda Misri wakiwa na ari kubwa.

"Hatutakuwa na muda mrefu wa maandalizi lakini nikwambie wachezaji wangu wana ari kubwa kuelekea mchezo huo"

"Tutasafiri kwa ndege hadi Cairo kisha tutapanda basi hadi mji wa Alexandria, muda ni mfupi lakini tumeshajiandaa hapa"

"Sasa tuna timu iliyoimarika zaidi ambayo inatupa nafasi ya kushindana na timu bora kama Al Ahly. Wachezaji wote tulisafiri nao wako tayari na tunakwenda kuipambania nembo ya Yanga," alisema Goncalves.

Yanga itasafiri kwa takribani masaa tisa ambapo masaa  matano watakuwa angani hadi Cairo ambapo hapo watachukua usafiri wa basi kuelekea mji wa Alexandria takribani masaa manne.

Mchezo dhidi ya Al Ahly utapigwa Ijumaa, saa 1 usiku kwa saa za Tanzania.

Yanga iliondoka mapema leo ikiwa na kikosi kilichojumuisha wachezaji 24.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
5h ago
READ MORE →
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
8h ago
READ MORE →
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
10h ago
READ MORE →
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
12h ago
READ MORE →
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
14h ago
READ MORE →
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
15h ago
READ MORE →
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
15h ago
READ MORE →
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
17h ago
READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
20h ago
READ MORE →
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE →