International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Jumatano Januari 21 2026

Joel JJ By Joel JJ
β€’
21 Jan 2026
Tetesi za usajili Ulaya, Jumatano Januari 21 2026

Aston Villa imeonyesha nia ya kutaka kumsajili mshambuliaji wa Crystal Palace na Ufaransa Jean-Philippe Mateta, 28, huku The Eagles wakimsaka mchezaji wa kimataifa wa Ivory Coast Evann Guessand, 24. (Athletic - usajili unahitajika)

Villa pia inaongeza juhudi za kumsajili mshambuliaji wa Roma Tammy Abraham, ambaye kwa sasa yuko kwa mkopo Besiktas, huku maafisa wa klabu hiyo wakimfuatilia mchezaji huyo wa kimataifa wa Uingereza mwenye umri wa miaka 28 akicheza mjini Istanbul Jumatatu. (Sky Sports)

Ajax inataka kumsajili Manuel Ugarte, 24, kwa mkopo huku ikimtafuta kiungo mkabaji lakini Manchester United haina mpango wa kumtoa mchezaji huyo wa kimataifa wa Uruguay. (Athletic- Usajili unahitajika)

Mkufunzi wa Borussia Dortmund Niko Kovac ameibuka kama jina jipya kwenye orodha ya Manchester United ya meneja anayefuata lakini kocha mkuu wa England Thomas Tuchel na Roberto de Zerbi wa Marseille wanasalia kuwa walengwa wawili wakuu. (Mirror)

Inter Milan inataka kumsajili mlinda lango wa Aston Villa Emiliano Martinez, 33, lakini mchezaji huyo wa kimataifa wa Argentina atalazimika kukubali kupunguziwa mshahara ili kusaini msimu ujao. (Sky Sports)

Muda wa mkopo wa Leon Bailey katika klabu ya Roma umekatizwa huku winga huyo wa Jamaica mwenye umri wa miaka 28 akirejea Aston Villa. (Sky Sports - kwa Kiitaliano)

Fulham itamenyana na Wolfsburg na Real Betis katika kinyang'anyiro cha kumsajili mshambulizi wa Jamhuri ya Ireland Troy Parrott, 23, kutoka AZ Alkmaar msimu wa joto. (Independent)

Kocha wa Coventry City, Frank Lampard anapigiwa upatu kuchukua nafasi ya Oliver Glasner kama meneja wa Crystal Palace huku klabu hiyo ikimtaka Jose Bordalas wa Getafe na Inigo Perez wa Rayo Vallecano. (Talksport)

Sunderland haina nia ya kumuuza kiungo wa kati wa DR Congo Noah Sadiki, 21, kwa Manchester United lakini ipo tayari kupokea ofa za wachezaji wasio na uwezo kama mkubwa vile kipa Mwingereza Anthony Patterson, 25, na kiungo wa kati wa zamani wa England aliye na umri wa chini ya miaka-20 Dan Neil, 24. (Sun)

Everton imemuulizia mshambuliaji wa Sunderland Mfaransa Wilson Isidor, 25, huku ikilenga kuimarisha safu yake ya ushambuliaji. (Mirro)

Beki wa Sheffield Wednesday, 17, Muingereza Yisa Alao anakaribia kujiunga na Januari klabu ya Chelsea. (Sheffield Star)

BBC

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
3h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
3h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
4h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
5h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
5h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
6h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
6h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
19h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
20h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
21h ago
READ MORE β†’